Sunday, December 11, 2016

Baraza la Biashara la Rastafari




RASTAFARI UNITED FRONT (RUF)
 
RASTAFARI BUSINESS FORUM (RBF)
Baraza la Biashara la Rastafari
Rastafari United Front (RUF) kiutendaji ipo kwa asilimia 80 kiuchumi zaidi, asilimia 10 Kiutetezi  na asilimia 10 kijamii hivyo itawajibika zaidi kuwa na sera madhubuti za kiuchumi mojawapo ni ile ya Baraza.la Biashara la Rastafari (RBF).    

Baraza la Biashara la Rastafari (RBF) ambalo limesajiliwa kama Bantu United Front (BUF) na BRELA na kupewa nambari ni utekelezaji wa RUF wa mpango wa Umoja wa Afrika kufikia mwaka 2063 kuinua kipato cha ndani cha mwananchi wa kawaida.

Lengo la RBF ni kuinua Jumuiya ya Rastafari kiuchumi na kubadili mtizamo wake na waweze kuendesha na kumiliki uchumi wake yenyewe ulioimarika na endelevu. RBF itawafanya Rastafari wawe na mwamko na kufuata kanuni bora za kifedha na kuwa na shule, vyuo, hospitali, na ardhi  yetu wenyewe kwa ajili ya makazi na kilimo na kuleta ushiriki mkubwa zaidi wa Rastafari katika maendeleo ya Taifa kiuchumi.
RUF katika kazi yake ya kuunganisha Rastafari  wote ina sera ya uchumi imara na endelevu kuanzia ngazi ya wilaya, mikoa, kitaifa na kibara 

Kazi hii ya kuunganisha imerahisishwa na Umoja wa  Afrika (AU) kwani katika mkataba wake wa Umoja na Utamaduni umechagua kutumia lugha ya Kiswahili kama lugha rasmi ya mawasiliano Barani Afrika.
Baraza la Biashara la Rastafari (RBF) litaweka mazingira ya kuingia katika uchumi wa Bara bara la Afrika kwa kuzalisha bidhaa zinazotokana na malighafi zetu na kuziwekea thamani na ubora utakaoshindana katika soko.

RBF inatoa fursa na mazingira ya ubunifu zaidi, kujiamini na maarifa ya kiuchumi kwa kutoa elimu ya ujasiriamali ili azalishe bidhaa zenye ubora na ushindani zaidi katika soko.

Sanaa kama muziki, sanaa za mikono, sarakasi, michezo, vichekesho, uchoraji, uchongaji na n.k. ni kazi na inahitaji itumike kikamilifu zaidi kama sehemu ya kuinua uchumi.

RBF itaweka mazingiza ya kutoa elimu ya ujasiriamali ili kuzalisha bidhaa zenye ubora. Ili tuwe na uchumi imara na endelevu ikishirikiana na mabaraza nchi jirani ya RBF ya katika kubadilishana uzoefu, utaalamu na bidhaa zinazozalishwa katika nchi husika. 

RBF itakuwa na ushirikiano na serikali ili kuweka mazingira mazuri ya kulinda haki miliki za wasanii, usafirishaji bidhaa nje na ndani, udhibiti wa bidhaa zisizo na viwango na ubora kuingia katika soko na unafuu wa malipo ya ushuru n.k. RBF itahamasisha Jumuiya za Rastafari kuwa na ushirika wa makampuni kama wanamuziki, wakulima, watayarishaji wa filamu na muziki, vyombo vya habari na Televisheni, usafirishaji, utalii, ukandarasi, ufundi mekanika, utunzaji wa mazingira, uvuvi na ufugaji n.k.

Hivyo mfumo wa utendaji kazi RBF utafanya kazi ya kutengeneza mtandao kama utando wa buibui kwa  kwenda nchi zote Barani Afrika na kuweka msingi mmoja wa RBF Afrika. 


No comments:

Post a Comment